BEATRICE WILLIAM
BELLA KOMBO
SARAFINA MSHINDO
WASHIRIKI wa shindano la kusaka vipaji la Bongo Star Seach ‘BSS’-Second Chance, kesho wanatarajiwa kutoa burudani katika Ukumbi wa Mzalendo Pub,imefahamika.
Washiriki hao watapanda katika jukwaa la ukumbi huo ambao leo hupambwa na usiku uliobatizwa kama ‘Fleva Nite’.
Msemaji wa Fleva Nite Boniventure Kilosa ‘Dj Venture’, alisema janja kwamba lengo la kuwapandisha jukwaani washiriki hao ni kutoa nafasi ya kuwaburudisha mashabiki watakaojitokeza katika ukumbi huo.
Alisema, wameshazungumza na waandaaji wa shindano hilo na kwamba shoo hiyo ni sehemu ya utaratibu wa shindano hilo kufanya maonyesho sehemu mbalimbali hadi kufikia hatua ya fainali ya shindano hilo hapo baadaye.
“Mambo yote yatakwenda kama kawaida tutapiga nyimbo za zamani na za sasa pamoja na washiriki hao wa BSS ‘kukamua’, naamini mashabiki watafurahia ‘shoo’ ya Jumamosi na waje waone mambo ya washiriki hao,” alisema Venture.
Comments
Post a Comment