RUFANI YA SHINYANGA UNITED

Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya Mwenyekiti wake Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Mstaafu Alfred Tibagana imekutana leo kusikiliza mashauri mbalimbali yaliyowasilishwa mbele yake.
Shinyanga United ilikata rufani kupinga kuenguliwa kwenye fainali hizo, uamuzi uliofanywa na Kamati ya Mashindano ya TFF baada ya klabu hiyo baada ya kutozingatia maelekezo ya TFF kuhusu usajili wa wachezaji wake.
Klabu hiyo ilipinga kuenguliwa ikieleza kuwa haikupata taarifa yoyote ya maandishi kutoka TFF ikiwazuia kuwatumia wachezaji ambao usajili wao ulikuwa na matatizo, na pia usajili wao ulifanywa na TFF.
Kwa uamuzi huo, Shinyanga United ambayo ilishika nafasi ya tatu katika Kituo cha Kigoma sasa itashiriki katika Fainali za Ligi ya Taifa zinazoanza keshokutwa (Agosti 6 mwaka huu) jijini Tanga.
Awali nafasi ya Shinyanga United ilikuwa imepewa timu ya Rumanyika SC ya Mkoa wa Kagera ambayo ilikuwa imeshika nafasi ya nne katika kituo hicho kilichokuwa na timu tano.

Comments