BABA WA OBI APATIKANA

BABA wa mchezaji wa Chelsea, Obi Mikel ambaye alikuwa ametekwa huko nchini Nigeria, amepatikana akiwa mzima, baada ya watekaji wake kumuachia. Baba yake huyo ambaye kwa muda wa siku 10 sasa alikuwa ametekwa na watu wasiojulikana, alipatikana akiwa mzima akiwa katika mji wa Kano, ambao upo Nigeria. Kwa mara ya mwisho baba yake huyo alionekana Agosti 12, akiwa katika mji mwingine wa Jos nchini Nigeria, ambapo gari alilokuwa akilitumia lilipatikana siku tano baadaye.
Taarifa iliyotolewa na kampuni ya SEM ambayo inamsimamia mambo yake ya utawala, ilikiri kupatikana kwa baba yake huyo na kusema kwa sasa yuko salama zaidi.
“Tunapenda kuufahamisha umma kuwa, baba wa Obi amepatikana akiwa mzima kabisa na anaendelea vizuri,” ilisema taaraifa ya kampuni hiyo.

Comments