YANGA KUJIPIMA NA POLISI DODOMA KESHO

WAKATI mabingwa wa soka wa kombe la Kagame pamoja na Ligi Kuu soka tanzania Bara wakiwasili mjini Dodoma leo, kesho wanatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya polisi Dodoma, mechi itakayopigwa kwenye dimba la Jamhuri Mjijini humo.
Yanga wamekwenda Dodoma kwa ajili ya kupeleka makombe hayo kwa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wanaendelea na vikao mjini humo, pia kuwapa fursa mashabiki wa huko kulishuhudia.
Aidha, kabla ya mechi hiyo, Yanga asubuhi ya kesho watatinga bungeni kwa ajili ya kupata mkono wa shukrani toka kwa wabunge.

Comments