YANGA KAMBINI

MABINGWA wa kombe la Kagame, timu ya soka ya Yanga inaingia kambini kesho kujiandaa na Ligi Kuu Ya Vodacom Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza kutimia vumbi Agosti 20 mwaka huu.
Kabla ya kuanxza kwa ligi hiyo ambayo Yanga ni mabingwa watetezi, wakali hao watacheza mechi ya kuwania ngao ya hisani dhidi ya Simba, mechi itakayopigwa Agosti 13 kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.Ikumbukwe kuwa, Yanga wanalishikilia kombe la Hisani.

Comments