TFF YAZIHIMIZA TIMU ZA LIGI KUU KUWASILISHA MAJINA YA VIWANJA ITAVYOTUMIA

Dirisha dogo la usajili litafunguliwa tena Novemba 1 hadi 30 mwaka huu.

Tunazikumbusha timu zote za Ligi Kuu kuwasilisha majina ya viwanja ambavyo
zitatumia kwa ajili ya ligi hiyo ambayo itaanza Agosti 20 mwaka huu.

 Klabu ambazo zimewasilisha maombi ya viwanja ambavyo zitatumia ni Mtibwa Sugar
(Manungu), Azam (Chamazi), Ruvu Shooting Stars (Mlandizi), Coastal Union
(Mkwakwani), Toto Africans (CCM Kirumba), Oljoro JKT (Kumbukumbu ya Sheikh Amri
Abeid Kaluta), Polisi Tanzania (Jamhuri, Dodoma) na Kagera Sugar (Kaitaba).

Klabu ambazo bado hazijawasilisha viwanja vyao ni Yanga, Simba, Moro United,
Villa Squad, JKT Ruvu na African Lyon. Timu hizo zinatakiwa kutuma majina ya
viwanja vyao haraka, kwani kabla ya kuruhusiwa kutumika ni lazima vithibitishwe
na Kurugenzi ya Ufundi ya TFF.

Comments