TFF KUWANOA WAAMUZI WA MIKOA YA DODOMA, MWANZA NA RUVUMA

Semina na mitihani ya utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wa 
daraja la pili na tatu itafanyika katika vituo vya Dodoma, Mwanza na Ruvuma 
kuanzia Agosti 2-5 mwaka huu. 
Waamuzi husika watajitegemea kwa usafiri, chakula na malazi. Tunavikumbusha 
vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kuwajulisha wahusika ili washiriki semina na 
mitihani ambayo pia itatumika kuwapandisha madaraja wale watakaofaulu.
 Semina kama hiyo kwa waamuzi wa daraja la IA na IB iliyoanza Julai 13 mwaka huu 
inaendelea katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza na itamalizika kesho (Julai 
16 mwaka huu).


Boniface Wambura
Ofisa Habari

Comments