TAIFA STARS KWENDA PALESTINA

Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania (Taifa Stars) itakuwa na ziara ya 
mechi mbili nje ya nchi. Stars itacheza mechi ya kwanza Agosti 10 mwaka huu 
mjini Ramallah, Palestina dhidi ya timu ya Taifa ya nchi hiyo.
 Stars ambayo inatarajia kuondoka Agosti 7 mwaka huu kwa ajili ya ziara ya mechi 
hizo mbili, itacheza mechi ya pili Agosti 13 mwaka huu dhidi ya Jordan katika 
Jiji la Aman. 
Kocha Mkuu wa Stars, Jan Poulsen ambaye hivi sasa yuko likizo kwao Denmark 
anatarajia kutangaza kikosi chake kwa ajili ya maandalizi ya mechi hizo mara 
baada ya kurejea nchini mapema mwezi ujao. 

Comments