MORO UNITED KUTUMIA UWANJA WA AZAM

Klabu ya Moro United imewasilisha barua ya kutumia Uwanja wa Azam ulioko 
Chamazi, Dar es Salaam kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom. Nayo Villa 
Squad imeomba kutumia uwanja huo huo, ingawa bado haijaonesha barua kutoka Azam 
inayowaruhusu kutumia uwanja wao.
 Klabu ya African Lyon ndiyo pekee ambayo bado haijawasilisha uwanja ambao 
itautumia kwa ajili ya ligi hiyo itakayoanza Agosti 20 mwaka huu. Kwa Lyon 
kushindwa kuleta jina la uwanja wake hadi sasa inasababisha TFF kuchelewa kutoa 
ratiba ya ligi, hivyo tunaitaka Lyon kutimiza wajibu wake katika suala hilo 
haraka.
 
 
Boniface Wambura 
Ofisa Habari

Comments