KOCHA MKUU WA SIMBA ATIMKA

KOCHA Mkuu wa Simba Mganda Moses Bassena ameondoka nchini kwenda kwao kwa mapumziko ya siku kadhaa kabla ya kurejea jumapili.
Basena ambaye timu yake ilishika nafasi ya pili katika michuano ya Kagame, ataanza kukinoa kikosi chake jumatatu ijayo ambacho kitaanza kujiandaa na michuano ya Ligi Kuu soka Tanzania Bara itakayoanza Agosti 20.
Kabla ya kuanza kwa ligi hiyo, Simba itakutana na Yanga Agosti 13 katika mechi ya kuwania ngao ya Jamii.

Comments