KLABU ZOTE ZA LIGI KUU BARA ZAWASILISHA USAJILI WAO TFF KWA WAKATI

Klabu zote 14 za Ligi Kuu ya Vodacom zimewasilisha usajili wa wachezaji wao kwa
ajili ya ligi hiyo iliyopangwa kuanza kutimua vumbi Agosti 20 mwaka huu. Mechi
ya kuzindua msimu kati ya Simba na Yanga itachezwa Agosti 13 mwaka huu Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.

Muda wa mwisho kuwasilisha usajili ilikuwa saa 6.00 usiku Julai 20 mwaka huu.
Klabu zote ziliwasilisha usajili wao Julai 20 mwaka huu kwa wakati na muda
waliowasilisha ukiwa ndani ya mabano.

Klabu hizo ni Ruvu JKT Stars (saa 9.00 alasiri), Oljoro JKT (saa 9.00 alasiri),
Kagera Sugar (saa 9.00 alasiri), Ruvu Shooting (saa 10.00 jioni), Polisi Dodoma
(saa 10.30 jioni), Moro United (saa 10.45 jioni), Simba (saa 1.30 usiku), Azam
(saa 3.45 usiku), African Lyon (saa 4.30 usiku), Yanga (saa 4.30 usiku), Villa
Squad (saa 5.30 usiku), Mtibwa Sugar (saa 5.40 usiku), Toto African (saa 5.50
usiku) na Coastal Union (saa 5.58 usiku).

Comments