JULIO AITA SILAHA ZA KUIANGAMIZA SHELISHELI(

U23 v SHELISHELI
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 23, Jamhuri
Kihwelo ametangaza orodha ya wachezaji 21 kwa ajili ya mechi za kirafiki dhidi
ya timu ya taifa ya Shelisheli.

Mechi hizo mbili zitachezwa Julai 27 na 30 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu
ya Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha.

Wachezaji hao ni Juma Abdul (Mtibwa Sugar), Himid Mao (Azam), Babu Ally
(Morani), Shabani Kado (Yanga), Salum Abubakar (Azam), Godfrey Wambura (Simba),
Jabir Aziz (Azam), Seif Juma (Ilala), Khamis Mcha (Azam), Shomari Kapombe
(Simba), Jackson Wandwi (Azam).

Wengine ni Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Thomas Ulimwengu (Humbarg SV, Ujerumani),
Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Mohamed Soud (Toto Africans), Jamal Mnyate (Azam),
Awadh Juma (Moro United), Salum Kanoni (Simba), Salum Telela (Yanga), Samuel
Ngasa (African Lyon) na George Mtemahanji (Modeva FC, Italia).

Boniface Wambura
Ofisa Habari

Comments