WIKI MBILI ZIMEBAKI KUPENDEKEZA BLOG/S UNAZOZIPENDA

Wakati uliobakia wa kupendekeza blog/s ni wiki mbili. Tunashukuru sana kwa ushirikiano wenu na tumefurahi kupata blogs nyingi sana katika Directory List yetu. Kama kuna blog hatujaiweka tafadhali usisiste kutuletea. Kuna mambo kadhaa yamejitokeza hivyo tunapenda kuchukua nafasi hii kuyaelezea inaelekea kuna watu hawajasoma sheria za mashindano yetu


1, Tafadhali unapojaza form ya kupendekeza blog/s zako jaza vipengele vichache tu sio zaidi ya vitatu unavyofikiri kuwa hiyo blog inazungumzia hayo mambo. Kuna watu wanajaza form na kuchagua vipengele vyote kwa blog moja tu. Tunajiuliza itakuaje blog moja iwe topic zake zinacover vipengele vyote? Hivyo tafandhali kuanzia sasa ukijaza zaidi ya vipengele vitatu utasababisha hiyo kura kupotea. Hatutaijaza kwenye list ya waliopendekezwa.

2. Tafadhali kama tulivyosema kwenye sheria zetu pia kama unataka kupendekeza blog/s tumia form hiyo hapo juu au tutumie email @ tanzanianblogawards@gmail.com na uandike ni vipengele gani hiyo blog/s unataka zishirikishwe. Ukiacha mapendekezo yako kwenye comments box kuanzia leo hatutazitafuta na kuziorodhesha. Kuna watu wanatutumia na kutuuliza je hii blog vipi au mbona blog fulani haipo mpaka sasa hivi. Ujue kuwa hatutengenezi hizo list tunazoziweka kila ijumaa. Tunacopy blog zilizopendekezwa na mtu kama wewe au yeyote yule..

3. Tafadhali usipendekeze forums. Forums sio blogs, tunaongeza kipengele cha blog zinazotumia picha au sauti kama podomatic lakini kama hatutapata watu wakutosha wakushiriki basi kipengele hicho kitaondolewa wakati wa kupiga kura.

Comments