TFF KULALAMIKA FIFA, KISA MRWANDA, BABI WAZUIWA KUJIUNGA NA STARS

DANNY MRWANDA
WACHEZAJI wa Tanzania wanaokipiga katika klabu  ya Dong Tam Long ya Vietnam Danny Mrwanda na Abdi kassim 'Babi' wameshindwa kujiunga na timu ya soka ya Taifa 'Taifa Stars' ambayo inajiandaa na mechi yake dhidi ya Afrika ya Kati itakayopigwa juni 5 huko Bangui.
Ofisa habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura amesema kuwa klabu hiyo  imekataa kuwaruhusu wachezaji hao kujiunga na Stars kwa madai kuwa iko kwenye hali ngumu katika ligi yao. Timu hiyo inashika nafasi ya mwisho kwenye ligi ya nchi hiyo inayoshirikisha timu 14, hivyo kudai kuwa wachezaji hao ni muhimu kwao kuwaokoa kutoka mkiani.

TFF tumepinga hatua hiyo kwa vile ni kinyume na Kanuni ya Hadhi na Uhamisho wa Wachezaji (Regulations of Status and Players Transfer), hivyo tutawasilisha malalamiko yetu kwa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Comments