YANGA YAMPIGA PINGU MIAKA MIWILI KIUNGO WA SIMBA

MABINGWA wa ligi kuu bara timu ya soka ya Yanga imemsainisha mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuichezea timu hiyo  aliyekuwa kiungo wa mahasimu wao wa jadi Simba, Rashid Gumbo.
Kazi ya kufunga pingu za kazi baina ya Gumbo na Yanga zilifanyika jana katika ofisi za mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga.
Zoezi hilo liliambatana na lile la beki wake Nadir Haroub 'Cannavaro'ambaye alibakiza mkataba wa mwaka mmoja sasa ameongezwa tena miaka miwili.

Comments