SIMBA SC YASHINDA RUFAA YA CAF, SASA KUKIPIGA NA WYDAD CASSABLANCA YA MOROCCO

WEKUNDU wa Msimbazi timu ya soka ya Simba imetinga katika ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya kushinda rufaa yake dhidi ya TP Mazembe ya Congo.
Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limeitupilia mbali mabingwa watetezi wa ligi hiyo Tp Mazembe kutokana na kumchezesha mchezaji ambaye hakusajiliwa na timu hiyo walipokwaana na Simba katika mechi ya wali iliyopigwa huko Lubumbashi, Kongo.
Kwa mantiki hiyo Simba sasa itakipiga na Wydad Cassablanca ya Morocco hivi karibuni na mshindi katika nmechi hiyo atatinga hatua ya nane bora.

Comments