MARADHI YANAYOTIBIWA NA KITUNGUU MAJI -2


Pumu:
Changanya juisi ya kitunguu maji na asali halafu kunywa kiasi cha kikombe kimoja, asubuhi na jioni. Endelea hivyo kwa muda wa mwezi mmoja.
Uvimbe wa pafu (Pneumonia):
Weka kibandiko cha kitunguu maji juu ya kifua na mgongo pamoja na kufunga kwa kitambaa, fanya hivyo kila siku kabla ya kulala.

Maradhi ya kinafsi:
Chemsha kitunguu na maganda yake, baadae mgonjwa wa kinafsi ale, au chukua juisi ya kitunguu maji na juisi ya saladi (lettuce) na kijiko kimoja cha asali changanya vyote ndani ya blenda na baadae unywe.

Saratani (Cancer):
Kausha maganda ya kitunguumaji kwenye jua, yasage na kiasi cha magamba hayo chukua magamba ya muoka (muoki, maloni, oak) halafu yakande katika asali na chukua na uchanganye katika juisi ya karoti (carrot) na unywe kiasi ya kijiko kimoja kwa muda wa mwezi mzima mfululizo, na baadae uvute moshi wa kitunguu maji kabla ya kulala.
Vidonda vya saratani:
Chukua juisi ya kitunguumaji kiasi cha kikombe, chukua na kiota (kiwawi, nettle) kamua majani yake kiasi cha kijiko kimoja na ongezea juisi ya kitunguu na halafu chukua hina iponde ndani yake ili ipate kuwa marhamu inayopakwa katika vidonda; fanya hivo kila siku pamoja na kunywa juisi ya kitunguu maji iliyochanganywa na juisi ya kiota kijiko kimoja kidogo na baada ya hapo kunywa kikombe kimoja cha maziwa.
Mvilio wa damu (Bruise):
Changanya juisi ya kitunguu maji pamoja na kiasi cha mafuta ya kafuri, sugua mahala pa mvilio asubuhi na jioni.
Majipu:
Saga kitunguu maji na kikange katika mafuta ya zaituni bila ya kuwa rangi ya manjano, paka kama marhamu na funga bendeji juu yake. Kila siku ukibadilisha pamoja na kusafisha utokaji wa usaha umalizike, halafu utakuwa ukitumia habasouda.

Chunusi:
Chukua kitunguu maji kisha ukisage, halafu ukikande katika unga wa ngano nzima, changanya na yai pamoja na mafuta ya simsim(ufuta) na upake usoni asubuhi na jioni pamoja na kula kitunguu kwa sana.
Ukurutu (Eczema):
Chukua juisi ya kitunguu na nanaa (mint) vipimo sawa, tengeneza kama krimu (cream) na ujipake baadae pangusa ukurutu kwa maji ya siki nyepesi, rudia kila siku pamoja na kujiepusha na kila kinachochea hisia. Kula matunda, mboga na asali kwa wingi.
Saratani ya ngozi:
Chukua juisi ya kitunguu maji, uwatu uliosagwa na salfa manjano kiasi cha robo kijiko kidogo; tengeneza marhamu jipake kila siku. Baada ya kuosha jioni jipake mafuta ya zetuni endelea hivyo kwa muda wa wiki.
ITAENDELEAAA..............

Comments

  1. asante mama pipiro kwa kutujuza mimi naomba kuuliza maana sijaelewa maana ya kinafsi ni kitu gani ni hilo pls naomba jibu

    ReplyDelete

Post a Comment