KASEBA AITOSA KICKBOXING, AGEUKIA NDONDI


BINGWA wa dunia wa mchezo wa kick boxing, Jahet Kaseba, ameamua kuupa kisogo mchezo ambao umempatia mafanikio makubwa.
Kaseba amesema kwamba moja ya mafanikio hayo ni kupatikana kwa mabingwa wengine wa kick boxing kama Kanda Kabongo na mwanadada Pendo Njau.
“Kwa hivi sasa nahamishia makali yangu katika mchezo wa ndondi ambapo naamini nitaweza kufanya vizuri zaidi kama ilivyokuwa kwenye kickboxing,” alisema.

Comments