WAPINZANI WA YANGA KUTUA ALHAMIS ALFAJIR, VIINGILIO NI SH.20,000 NA 3,000

LOUIS SENDEU, MSEMAJI WA YANGA
TIMU ya Dedebit ya Ethiopia inatarajiwa kuwasili nchini Alhamis Alfajir kwa ndege ya Shirika la Ethiopia tayari kwa mechi yake na Yanga itakayopigwa jumamomosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Msemaji wa Yanga Louis Swendeu ametaja viingilio katika mechi hiyo ni sh.20,000 kwa watakaokaa jukwaa la VIP A, sh.10,000 kwa VIP B, sh.5,000 kwa jukwaa la orange na sh.3,000 kwa jukwaa la kijani.

Comments