PETER MSECHU AZAWADIWA BIMA YA AFYA NA KAMPUNI YA PREMIER PLAN

Meneja Mkuu wa Resolution Health Afrika mashariki, Oscar Osir, akimkabidhi msanii Peter Msechu zawadi ya bima ya afya kiwango cha Premier Plan kutona na mchezo alioshiriki wa Tusker Project Fame 4 mwishoni mwa mwaka jana. Hafra hii ilifanyika ofisi kuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Peter Msechu akiwa na wafanyakazi wa kampuni ya bima ya afya Resolution Health wakiwa katika ofisi kuu ya kampuni jijini Dar es Salaam baada ya kupokea zawadi ya bima ya afya kiwango cha Premier Plan ambayo itadumu mwaka mzima wa 2011.

Peter Msechu akiipongeza kampuni ya bima ya afya Resolution Health, kutokana na zawadi aliyopokea toka kampuni hiyo ya Bima ya Afya kiwango cha Premier Plan ambayo itadumu mwaka mzima wa 2011. Pembeni ni Meneja Mkuu wa kampuni, Bwana Oscar Osir, katika hafra iliyofanyika ofisi kuu ya kampuni, jijini Dar es Salaam jana.

Comments