WANACHAMA TASWA KALIPENI ADA YA MWAKA


AMIR MHANDO, KATIBU MSAIDIZI WA TASWA

CHAMA cha waandishi wa habari za michezo Tanzania (TASWA) kimewataka wanachama wake kulipia ada ya mwaka ili kuweza kushiriki katika mkutano mkuu wa uchaguzi unaotarajia kufanyika Agosti 7jijini Dar es Salaam.

Katibu Msaidizi wa TASWA, Amir Mhando amesema ada hiyo ya shilingi elfu 20 mwisho wa kuipokea itakuwa ni Julai 31.

Alisema zoezi la utoaji fomu kwa wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali za uongozi litaanza Agosti mbili mpaka Agosti na nafasi zitakazowaniwa ni pamoja na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu, Katibu Mkuu Msaidizi, Mweka Hazina, Mweka Hazina Msaidizi na Wajumbe sita wa kamati ya utendaji.

Comments