UONGOZI MPYA YANGA KUPATA BARAKA ZA WAZEE KESHO


BAADHI YA VIONGOZI WAPYA WA YANGA PAMOJA NA MDHAMINI WA KLABU HIYO, YUSUF MANJI NA MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI, RIDHWAN KIKWETE

UONGOZI mpya wa klabu ya Yanga leo unatarajiwa kukutana na wazee wa klabu hiyo kwa ajili ya kujitambulisha rasmi sambamba na kupata baraka zao.



Kupitia kikao hicho kitakachofanyika makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo mitaa ya jangwania na Twiga kuanzia saa nane mchana, viongozi hao pia watapokea mapendekezo yoyote toka kwa wazee hao.


Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisa habari wa Yanga, Louis sendeu alisema kwamba, lengo la mkutano huo pia ni kuweka ukaribu baina ya pande hizo mbili kwani ushirikiano na baraka ni muhimu katika utendaji wao.


Viongozi hao walipatikana kupitia uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa PTA junmapili iliyopita ambapo Llyod Nchunga alichaguliwa kuwa mwenyekiti na Davis Mosha alitwaa nafasi ya makamu mwenyekiti.


Aidha walipatikana wajumbe nane ambao ni pamoja na Ally Mayai, Mzee Yusuf, Salim Rupia, Charles Mugondo, Mohamed Bhinda, Sarah Ramadhan, Teonest Rutashoborwa na Tito Osoro.

Comments

  1. Msema kweli ni mpenzi wa mungu Dada dina sema ukweli wako wewe ni yanga damu? kwani hatupumui na habari za jangwani
    mdau
    James
    Holland

    ReplyDelete
  2. Mesekweli ni mpenzi wa mungu Dada dina ebu tuambie ukweli wewe ni yanga damu? kwani hatupumui na habari za jangwani.
    Mdau
    James
    Holland

    ReplyDelete
  3. James, mimi ni mwandishi wa habari za michezo na burudani hivyo naweka habari zilizopo,au vibaya?

    ReplyDelete
  4. Sawa Dada Dina nimekubali yaishe. endelea kutuletea burudani si unajua sisi tupo ughaibuni lkn tukipata habari za nyumbani tunafarijika sana.
    Mdau
    James
    Holland

    ReplyDelete

Post a Comment