BONGO STAR SEARCH 2010 YAZINDULIWA

MADAM RITHA

SHINDANO la kumsaka nyota wa muziki la Bongo Star Search (BSS) kwa mwaka 2010 linatarajiwa kuanza Julai 17 hadi Agosti 12 na kufanyika katika mikoa minne.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Benchmark Productions Rita Paulsen inayoendesha shindano hilo alisema wameamua kupunguza mikoa kutokana na kutotoa wasanii wenye vipaji hivyo mikoa iliyobahatika kusaka wasanii ni pamoja na   Arusha, Dodoma, Mwanza na Dar es Salaam.

MADAM RITHA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO KATIKA UKUMBI WA IDARA YA HABARI (MAELEZO)
Alisema vipindi vitaanza kurushwa katika kituo cha televisheni cha ITV kuanzia Agosti 28 na kuendelea katuika siku za jumapili mpka shindano litakapofikia tamati..

Comments