SUGU
WASANII wakongwe nchini wanaoimba muziki wa Hip Hop akiwemo JOseph Mbilinyi 'mr sugu', Fred Maliki 'Mkoloni na Gerald Mwanjoka 'G.Solo' ambao ni wanaharakati katika masuala mbalimbali ya kutetea jamii wametangaza kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
G.SOLO
Wakitangaza maamuzi hayo kwa wanahabari katika makao Makuu ya CHADEMA walisema wamefikia uamuzi huo ili kutimiza adhima yao ya kuwatetea wanyonge.
MKOLONI:"Nimeona ni bora kuziongezea nguvu harakati zangu kupitia CHADEMA kwani dhamira na maudhui yake yanaendana nacho"
MKOLONI
SUGU: "nimekuwa nikitafakari kwa kipindi kirefu kipindi kirefu ni chama gani makini chenye nguvu ya kuwatetea wanyonge na hapa ndio mahali pake, hivyo natumaini dhamira yangu itatimia".
Mwisho. b
Comments
Post a Comment