KIPAJI REDD'S MISS ILALA KUSAKWA KESHO

                            
WASHIRIKI MISS ILALA 2010

SHINDANO  la kutafuta mrembo mwenye kipaji zaidi kati ya Warembo wanaoshiriki kinyang’anyiro cha kumtafuta Redds Miss Ilala litafanyika Jumanne tarehe 22 june kuanzia saa tatu usiku katika Ukumbi wa Lamada Hotel Apartment.


Warembo watakao chuana wamerejea jijini kutoka katika ziara ya kitalii na mafunzo mkoani Tanga ambako walihudhuria pia mashindano ya Miss Tanga ambayo yalikuwa na shindano dogo la vipaji. Naamini wamejifunza kutoka kwa wenzao wa Tanga, wameona mapungufu yao pia watakuwa wameona namna ya kuonyesha vipaji.

Kwa muda wa wiki mbili wamekuwa wakijifua wakijiandaa kwa shindano hili ambalo tunaona kuwa litakuwa na ushindani mkubwa ikizingatiwa kuwa wataalam waliobobea walifika kambini kuwafunda na kuwaendeleza katika kukuza vipaji vyao.

Wataalamu waliofika kambini kuwafunda Warembo ukiacha Mwalimu wao wa vipaji Torry Oscar ambaye ni Mshindi wa Vipaji kwenye Miss Tanzania 2009/10, ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Nyumba ya Vipaji (THT), Ofisa utamaduni wa Manispaa ya Ilala Shani Kitogo na Mwana muziki Rina kutoka Tanzania House of Talent
Shindano hili ambalo litahudhuriwa tu na wageni waalikwa ikiwa ni wazazi, wadhamini, na watu maalum .

Warembo watakaowania taji hilo ni Happyness Mushi ( Kucheza muziki na kuimba), Sarah Nalolah (Kucheza),Salma Mwakalukwa (Kucheza muziki),Doreen Mutabingwa (Kucheza muziki),Lilian Hassan (Kutangaza na Kucheza), Cinthia Bavo (Kuimba),Consolatha Lukosi (Kucheza Muziki), Ritha Swai ( kucheza),Ummy Mohamed (Kucheza Taarabu) Neema Salawa ( Kucheza mpira wa Miguu),Harrieth Mulumba ( Kuigiza), Sarah Mukajanga ( Kuimba na Kucheza),Agness Francis ( kucheza muziki), Mariam Kimario ( Kucheza).,Nema Allen (Kuimba), Bahati Chando (Kucheza muziki),Celine Wangusu ( Kucheza).
Mchuano wa vipaji kwenye mashindano ya Redds Miss Ilala ni kuendeleza na kutimiza dhana ya Wandaaji wa Miss World wanaosisitiza suala hili la “urembo na Vipaji” Mwaka uliopita, shindano la kutafuta Mrembo wa dunia, lililofanyika Afrika ya kusini lilipambwa na washiriki wa Miss World wenye vipaji pekee.

Shindano la Redds Miss ilala litakalofanyika Jumamosi ijayo katika ukumbi wa Ubungo Plaza litapambwa na kuburudishwa na Shoo za Warembo, FM Academia ( Watoto wa Mjini )na Wanne Star.

Jumanne mchana kabla ya shindano la Vipaji, Warembo watatembelea Tanzania Breweries Limited kwenda kujifunza namna ya Kinywaji cha Redds kinavyotengenezwa na mambo mbalimbali yanayohusu Redds original premium.

WADHAMINI:
Redd's Premium Original, Vodacom Tanzania Lamada Hotel Apartment, Channel Ten, Aurora Security, valye spring, Fabak Fashin, Habari Leo, Clouds FM, Muzasha Tours,Sofia Production, Jambo Leo, Cxc Africa, Fullshangwe blogspot, Issamichuzi blogspot na Syscorp Group

Comments