KUTOFANYIKA TAIFA CUP KUMEUA HAMASA YA SOKA MIKOANI

Na Dina Ismail
KWA karibu  takribani miaka minne sasa, michuno ya soka ya kombe la Taifa  maarufu kama ‘ Taifa Cup’ imeshindwa  kufanyika.
Michuano hiyo ambayo ambayo ilianzishwa waka 1964 ikijulikana kama  Sunlight Cup ilikuwa na lengo la  la kuvumbua na kukuza vipaji vya  vilivyojificha katika mikoa hiyo.
Pia michuano hiyo ililenga kuamsha na kuhamashisha michezo na hasa mpira wa miguu katika mikoa hiyo kwa lengo la kupata wachezaji ambao baadae wataunda kikosi cha timu ya Taifa ya Bara ambacho kitaiwakilisha nchi katika michuano ya Chalenji.
Kupitia michuano hiyo tumepata kushuhudia kuibuka kwa wachezaji mbalimbali ambao leo hii wameweza kuandika historia katika ramani ya soka hapa nchini.
Kama hiyo haitoshi mivhuano hiyo imeweza kuleta hamasa kwa hata baadhi ya mikoa ambayo imekuwa haisikiki katika medani ya soka kuamka kutokana na kuunda timu ambayo inauwakilisha mkoa katika michuano hiyo.
Aidha michuano yab kombe la Taifa, inatumika pia kuleta umoja, ushirikiano na upendo sambamba na burudani ambayo baadhi ya mikoa imekuwa ikiikosa kutokamna na kukosa kushuhudia michuano mbalimbvali na hasa ya ligi kuu bara.
Chini ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) michuano hiyo imekuwa ikifanyika  na kuna nyakati imeshindwa kufanyika kutokana na sababu mbali mbali na hasa kukosekana kwa wadhamini wa michuano hiyo.
Mara ya mwisho michunao hiyo ilifanyika mwaka 2011 ambapo kampuni ya bia Tanzania (TBL) ilikuwa ikiidhamini michuano hiyo kupitia vinywaji vyake tofauti kuanzia mwaka 2005.Mara ya mwisho ilifanyika mwaka 1994.
Hata hivyo, mpaka sasa TFF imeshindwa kabisa kufanya jitihada zozote za kuhakikisha michuano hiyo inarejea tenja ili kurejesha hadhi ya kabumbu hapa nchini.
Kwamba, kuna  mikoa  ambayo haina timu zinazoshiriki Ligi Kuu  mfano mkoa wa Singida ‘Kindai United’uliotwaa ubingwa huo mwaka 2010, iliweza kutoa upinzani mkubwa na hata kutwaa kombe.
Kama hiyo haitoshi hata katika usajili wa wachezaji kulikuwa na ushindani wa hali ya juu kama usajili wa ligi kuu bara ambako baadhi ya wachezaji walijikuta wakigombaniwa na mikoa zaidi ya mmoja na mwisho wa siku suala la kucheza wapi lilibaki kwa mchezaji.
Raha ilikuwa kwa timu ya mkoa wa Dar es Salaam ‘Mzizima United’  katika usajili kusheheni nyiota wengi wanaocheza ligi kuu bara na hasa Simba na Yanga, kabla ya baadaye kugawanywa katika mikoa mitatu yaani Temeke, Ilala na Kinondoni.
Kupitia michuano hiyo ambayo ilikuwa na msisimko wa aina yake, tulipata kuona ushindani wa hali ya juu toka kwa timu shiriki ambapo kila mkoa ulijitahidi kusajili wachezaji wazuri ambao waliweza kutoa ushindani mkubwa kwa timu pinzani.
Kwa vile michuano hiyo ilikuwa inafanyika kipindi ambacho ligi imesimama, baadhi ya vilabu pia viliitumia kupata wachezaji ambao iliwasajili katika vilabu vyao.
Kwa mantiki hiyo, tangu kusimama kwa michuano hiyo hamasa ya soka imekosa msisimko zaidi imebakiki kwa mechi za Simba na yanga tu kidogo na timu ya Taifa.
Hivyo  ni vema kwa TFF kufanya kila liwezekano kwa kuongea na makampuni makubwa  ambayo yataweza kusaidia kufanyika kwa  michuano hiyo kwa mara nyingine na  fursa  kwa  wadau wa soka mikoani kupata burudani ya aina yake.
Hawa ndio mabingwa wa Taifa Cup  Pwani ( 1964), Tanga (1965), Kilimanjaro (1966), Pwani (1967, 1968), Tanga (1969), Morogoro (1970), Kilimanjaro (1971), Pwani (1972),Tanga (1973), Morogoro (1974)Dar es Salaam (1975,1976,1977), Kilimanjaro (1981,1983), Mwanza (1984,1985), Dar es Salaam (1986,1987,1998).

Mwak 1999 hadi 2004 haikufanyika kabla ya mwaka 2005 Mbeya kuwa bingwa, 2006/2007 bingwa alikuwa Dar es Salaam, Ilala (2008, 2009), Singida (2010) na Mbeya  (2011).

Comments