OMOG ALIPIGA CHINI UJIO WA OKWI SIMBA



Na Dina Ismail
LICHA ya uongozi wa Simba kutaka kumrejesha mshambuliaji  wa kimataifa Mganda Emmanuel Okwi, kocha mkuu wa timu hiyo, Mcameroon Joseph Marius Omog  hajakubaliana na hilo.
Habari za kuaminika kutoka klabu ya Simba zinaeleza kwamba, Omog kabla ya kuondoka alipendekeza majina ya wachezaji ambao anataka wasajiliwe na katika hiyo orodha hakukuwa na jina la Okwi.
Imeelezwa kwamba katika ripoti ya Omog, amepanga kuleta kipa na mshambuliaji  kutoka nchini Ivory Coast kwa ajili ya kukiimarisha kikosi cha timu hiyo katika mzunguko wa pili wa ligi kuu bara.
Omog ambaye alikwenda likizo  kwao baada  kumalizika kwa mzunguko wa pili ulioiacha Simba katika nafasi ya kwanza, anatarajiwa kurejea nchini wakati wowote kuanzia sasa kwa ajili ya kuendelea kukinoa kikosi chake.
Simba ambayo ilimuuza Okwi mwaka juzi kwa dau la dola 100 katika klabu ya Sonderjiske ya Denmark. ilipanga kumrejesha Okwi  kwa dau la dola za Marekani 120,000 ( zaidi ya Sh milioni 240).
Hata hivyo, habari zinaeleza kwamba, licha ya kocha kutompendekeza Okwi katika usajili wake, uongozi wa Simba umeona  dau lake ni kubwa ukilinganisha na kiwango alichonacho kwa sasa.
“Haiwezekani  Okwi kununuliwa kwa gharama hiyo, yaani tumuuze kwa dola 100 halafu tumnunue kwa dola 120 kwa kiwango gani zaidi, kwanza kocha hajamtaka  na amepanga kuleta mshambuliaji mahiri kutoka Ivory Coast, alisema kiongozi huyo

Okwi  alipata kujiunga Simba kwa mara ya kwanza mwaka 2010 na kuiwezesha kutwaa mataji kadhaa kabla ya mwaka 2013 kuzwa  Etoile du Sahel ya Tunisia dola 300,000.

Comments