MAKOCHA LIGI KUU WANAUA VIPAJI VYA SOKA


Na Dina Ismail
WAKATI mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara unatarajiwa kuanza leo, dirisha dogo la usajili kwa timu shiriki linafungwa rasmi lilifungwa rasmi juzi huku tukishudia kila timu ikijaribu kufanya mabadiliko.
Kwa wiki kadhaa tumekuwa tukisikia habari za usajili wa wachezaji mbalimbali ambao wanadaiwa kuachwa ama kuhitajiwa na timu hizo.
Kila timu ilikuwa katika harakati za kusajili wachezaji ambao inadhani uwepo wao utaziwezesha timu zao kufanya vema katika ligi hiyo na michuano mingine na hatimaye kutwaa ubingwa.
Zoezi  la kuacha au kusajili mchezaji linafanywa na viongozi wa timu wakifuata mapendekezo ya makocha wa timu husika.
Lakini shughuli inakuja kipindi cha Ligi kwani makocha wanashindwa kuwa ‘fair’ katika matumizi ya wachezaji  katika michezo mbalimbali.
Hii ina maana kwamba, makocha ndio waliowataka wachezaji hao wasajiliwe katika timu zao, lakini matokeo  hushindwa kuwatumia ipasavyo hivyo kuonekana mizigo.
Kwamba, kocha alimuona mchezaji fulani anafaa na akaagiza asajiliwe na tena wengine huasajiliwa kwa kiasi kikubwa cha fedha lakini na baada ya kuanza kwa ligi kocha anashinda kumtumia.
Kuna baadhi huwa na bahati kwa kuwa mchezaji chaguo la kwanza msimu mzima, wengine hujikuta mchezaji wa akiba na wengine sasa huishia mazoezini tu.
Sasa hali ya kusajili mchezaji na kutomtumia ni kama na ufujaji wa pesa na pia kuua kipaji cha mchezaji.
Kwani, ni bora usajili wachezaji wachache ambao unaamini watakufaa katika ligi na pesa nyingine itumike kwa matumizi mengine au kumsajili mchezaji ambaye atapata nafasi ya kucheza na kuendeleza kipaji chake.
Wenzetu nchi zilizopiga hatua tumeona wachezaji wakicheza kwa kupiokezana yaani hakuna wasugua benchi wa kudumu na ndio maana wanapata mafanikio makubwa.
Lakini kwa hapa Tanzania naweza kusema makocha ndio wanaua vipaji vya wachezaji kwani naamini kuna wachezaji ni wazuri tu tunawaona kwenye mazoezi lakini hawapewi nafasi sana wakibahika kucheza ni mchi za kirafiki.
Mpira ni ajira, kama mchezaji hafai ni bora kumuacha aende sehemu inayomuhitaji akacheze na maisha yaendelee kuliko kumsugulisha benchi na matokeo yake hata kipaji kinaishia benchi;ndiyo mchezaji hata kama anakipaji kikubwaa akikaa benchi sana anajikuta anapoteza mwelekeo.
Mchezaji amepambana mpka kufikia hatua ya kucheza ligi kuu bara, anasajiliwa na kupewa kitita kizuri tu, lakini mwisho wa siku anashindwa kutimiza wajibu wake sababu ni kocha kutompanga.
Ifikie mahali makocha nao wawe na roho za kibinadamu kwani kama nao wangefanywa hivyo hii leo wangekuwa makocha?
Nadhani tutarajie mabadiliko ya upangaji wa vikosi katika mzunguko huu wa pili uwe wa  haki na usawa na si upendeleo kama inavyodhaniwa ili kuendeleza na kukuza vipaji.
Kuna timu zimepandisha wachezaji vijana ni vema wakapewa nafasi za kucheza mara moja moja ili kuwapa uzoefu kwani bila kufanya hivyo watatoa wapi uzoefu.
Kila la heri makocha wa timu shiriki, George Lwandamina (Yanga), Joseph Omog (Simba), Ali Bushir (Mwadui), Suleiman Matola (Nanda Fc), Ettiene Ndalyagije (Mbao Fc), Mecky Mexime (Kagera Sugar), Kinnah Phiri (Mbeya City) na Athuman Bilal (Stand United).

Pia wapo Salum Mayanga (Mtibwa Sugar), Zeben Hernandez (Azam Fc), Kally Ongala (Majimaji), Hamimu Mahadh (Tz Prisons), Fernando Jose Bernado Tavares ( African Lyon),Jurgen Seitz (Toto African) na  Malale Hamsini (Ruvu Shooting).

Comments