TASWA WAMPONGEZA CHEKA

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kinatoa pongezi kwa bondia Francis Cheka kwa kuibuka bingwa mpya wa dunia wa WBF katika uzito wa Super Middle.
Cheka alitwaa mkanda huo wa ubingwa baada ya kumshinda Mmarekani, Phil Williams kwa pointi katika pambano la raundi 12, lililofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Ijumaa usiku.
TASWA imekunwa na mafanikio hayo na inatoa pongezi za dhati kwa bondia huyo kwa juhudi zake na kulitangaza vyema jina la nchi yetu, hivyo tunasema Cheka atambue familia ya wanamasumbwi na wanamichezo wote Tanzania tumefurahishwa na mafanikio hayo na tunayajali.


Comments