Skip to main content

KUELEKEA MISS TANZANIA USIKU WA LEO:HAPPINESS WATIMANYWA MMOJA YA WASHINDANI




Kama ni mfuatiliaji mzuri wa kipindi cha Skonga, utamkumbuka Happiness Watimanywa, msichana pekee kutoka Tanzania aliyeweka historia ya kuongoza nchi zaidi ya 150 za mtandao wa IGCSE katika somo la Uhasibu kwenye mitihani ya kidato cha nne mwaka 2010.


Happy (19) ni mzaliwa wa familia ya kawaida sana ya Mr Louis Roussos ya Morogoro. Wadogo zake Angel na Romeo sasa wanasoma St. Constantine shule iliyomtoa Happy. Pia, Happiness Watimanywa amewahi kusoma Laureatte International School ya Dar-es-salaam, ambapo akiwa hapo, alikutana na mwalimu wa michezo Mr Tchalewa Ndeki ambaye alimfungulia mipaka mingi Happy. Akiwa Laureatte, Happy aliwahi kwenda China na South Korea akiwa na wanafunzi wenzake katika matamasha mbali mbali ya elimu na michezo. Baada ya kumaliza kidato cha nne, Happy alifanikiwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Strathclyde cha UK ambapo anasomea digrii ya Biashara.





Kipindi ambacho Happy yupo kwenye likizo ndefu, alipata wakati mgumu wa kutokuwa na kitu cha kufanya, hivyo Happy aliamua kujihusisha na masuala ya urembo na kufanikiwa kutwaa Taji la Miss Dodoma, na Miss Kanda ya Kati na hatimaye kuingia kwenye kambi ya Miss Tanzania.



Akiwa Miss Tanzania, Happy alikuwa ni mshiriki wa kwanza kuingia Nusu Fainali ya mashindano hayo kwa kutwaa taji la Redds Miss Photogenic 2013.




Ndani ya kambi ya Miss Tanzania, Happiness Watimanywa amekuwa mwiba kwa warembo wengine 29 wanaowania taji hilo kwani amekuwa akionesha uwezo wa hali ya juu kuanzia kwenye kipaji hata michezo, ukiachilia mbali upeo mkubwa alio nao.

Leo ndio leo ambapo Happy anatarajia kudhihirisha kuwa pamoja na elimu na uwezo mkubwa alio nao, pia ni mrembo. Tusubiri matokeo ya Redds Miss Tanzania 2013.

Comments