AZAM FC, ASHANTI KUPIMANA UBAVU KESHO CHAMAZI COMPLEX

TIMU za Azam Fc na Ashanti United zinazoshiriki Ligi Kuu Soka Tanzania Bara kesho zitamenyana katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu utakaofanyika katika dimba la Chamazi Complex.
Msemaji wa Azam Fc iliyoandaa mchezo huo, Jaffer Iddy amesema leo kwamba mchezo huo ni maalum kwa kuzipima nguvu timu hizo ambazo kwa sasa zipo katika mapumziko mafupi ya ligi hiyo.
Alisema mchezo huo utakaoanza majira ya saa 10 jioni hautakuwa na kiingilio hivyo amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi.

Kwa upande mwingine, Maganga amesema kwamba wachezaji wake waliokuwa majeruhi John Bocco ‘Adebayor’ na Aggrey Morris hali zao zimeimarika na tayari wameanza mazoezi mepesi.

Comments