MICHAEL WAMBURA AUNGA MKONO MSAJILI KUGOMA KUISAJILI MAREKEBISHO YA KATIBA YA TFF


Katiba ya TFF ya 2012 ilifutwa na msajIli wa vyama vya michezo na vilabu kwa kuwa ilibadilishwa kinyume cha sheria(BMT)  pamoja na Katiba ya TFF ibara ya 30  kwa kutumia njia ya waraka badala ya Mkutano Mkuu,  hivyo katiba halali kisheria inayotambulika ni ile ya 2006 na mabadiliko yake . FIFA  na Serekali kupitia wizara yenye dhamana na  michezo iliiagiza  TFF iitishe Mkutano Mkuu ili ifanye mabadiliko ya katiba stahiki kwa mujibu wa katiba  na  kwa kufuata taratibu zilivyoainishwa  kwenye katiba ya TFF. Nimelazimika kuendelea kuiunga mkono Serikali kupitia  msajili  kwa maamuzi yake ya kukataa kusajili mabadiliko  ya katiba ya TFF kwa kuwa TFF  kwa makusudi   imeendelea kuvunja katiba yake katika kufanya mabadiliko.
Kisheria  msajili husajili mabadiliko yoyote ya Chama kilichosajiliwa chini ya Sheria ya BMT kwa kuzingatia  Sheria NA 12 ya 1967 na marekebisho yake NA 6 ya 1971 ya Baraza la Taifa la Michezo pamoja na  Kanuni za Baraza la Michezo la Taifa  na Kanuni za  Usajili NA 422 za1999.
 Chama chochote kitakacho kwenda kinyume na sheria hizo hikiwezi kupewa usajili au Katiba yake na marekebisho yake hayawezi kupewa usajili,aidha uamuzi wa msajili   sio tu utaifanya TFF peke yake itambue sheria  bali hata vyama vingine vitawajibika kufuata utaratibu katika kufanya mabadiliko ya katiba zao,
Katiba ni nyaraka ya kisheria hivyo chombo chenye mamlaka kisheria hapa Tanzania ya kutafsiri katiba ni Mahakama pale pande mbili zinapotofautiana juu ya tafssiri ya Katiba, hivyo kwa kufanya hivyo msajili atakuwa ameepusha suala la Katiba ya TFF kuingia katika mikono ya kimahakama kwa kuwa utaratibu uliotumika kubadili katiba ya TFF  ni dhahiri haukufuata taratibu zilizoainishwa kwenye katiba ya TFF  na sheria na  za nchi kama zilivyoaanishwa. Sababu kuu zinazonipelekea mimi kuunga mkono uamuzi huo ni kama zifuatazo:

1.   UPIGAJI KURA MAREKEBISHO YA KTIBA
 Ibara ya 30(4) ya katiba ya TFF 2006 inaelekeza ya  kuwa  mapendekezo ya mabadiliko ya katiba ya yatapitishwa ikiwa yataridhiwa na wajumbe theluthi mbili(2/3)  ya wajumbe   wenye haki ya kupiga kura.
·         Ibara ya 28(4) maamuzi yote ya mkutano mkuu yatafanywa kwa  kuzingatia uwingi wa kura halali  zitakazopigwa na wajumbe halali wa Mkutano  Mkuu  labda  ikiwa katiba ya TFF inaelekeza vinginevyo. “ Unless otherwise stipulated in the statutes the decisions of the general assembly shall be taken by simple majority  of the votes validly cast by the official delegates”.
·         Ibara 28(5) ya katiba ya TFF(MAAMUZ) 
Inazungumzia Maamuzi  yanayohusiana na mabadiliko yoyote ya makao makuu ya TFF, mabadiliko yoyote  ya Katiba na Kanuni zake, marekebisho yoyote  ya ajenda kwenye mkutano mkuu wa kawaida, maamuz iyoyote  yanayohusiana na kusimamishwa au kufukuzwa mjumbe wa vyombo vya TFF au inayohusiana na kuvuliwa hadhi ya Urais wa heshima  au mwanachama wa TFF au inayohusiana na kutengwa kwa mwanachama  au kuvunjika kwa TFF lazima itahitaji   zaidi ya 2/3 ya kura halali zililizopigwa na wajumbe  resmi wa Mkutano Mku               “ Decision relating to any change of head office  of TFF ,any amendments of Statutes and regulations, any modification to the agenda  of the ordinary general assembly, any decision relating to  suspension or dismissal of member  a member of  an organ of TFF or  relating to bestowing of the title of honorary president or member of the TFF or relating to the exclusion of a member of TFF or dissolution of TFF shall require a majority of 2/3 of the votes validly cast by the official delegates”.
Kwa kuwa hakuna kura zilizopigwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF  na kuhesabiwa  kuamua ama kupitisha au kukataa mabadiliko basi zoezi hilo na marekebisho hayo ni batili kwa mujibu wa Katiba ya TFF.

2.   MKUTANO MKUU WA DHARURA
Ibara ya 25(4) katiba ya TFF ya 2006 inaelekeza kuwa  Agenda  na makabrasha ya Mkutano Mkuu ni lazima yawafikie wajumbe wa mkutano mkuu walau siku  15 kabla ya mkutano Mkuu.
 Kwa kuwa wajumbe walipewa agenda na makabrasha siku moja kabla ya Mkutano Mkuu,  huo ulikuwa uvunjaji mkubwa wa Katiba ya TFF , wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF hawajiwakilishi wao bali  wana wakilisha Mikoa, Vyama shirikishi na Vilabu  ambavyo  vina wanachama wake na kamati zake za utendaji ambazo zilikuwa na haki ya kujadili na kuwapa wawakilishi wao mawazo yao kwani maamuzi ya ya TFF yanagusa kuanzia  ngazi ya Taifa mpaka wilaya.
3.   KUINGIZA VIFUNGU KWENYE KATIBA BILA KUJADILIWA NA KUPITISHWA NA MKUTNO MKUU WA TFF
Kwa kuwa marekebisho ya  katiba kwa kutumia waraka  ya 2012 yaliyowasilishwa kwa msajili, usajili wake ulifutwa hiyo maraekebisho yote yaliyofanyika wakati huo ikiwa ni pamoja ibara Ibara 52 (1(b),2,3,4,5,6(a,b)  yanayohusu  Kamati ya Uchaguzi na kamati ya Rufaa ya  Uchaguzi iliyopelekea Uteuzi wa  Mtinginjola na kamati yake  , pamoja na   Ibara ya 64(1,2) ya leseni za vilabu yanakuwa  batili, hivyo  kama TFF ilikuwa  bado  inapenda vifungu hivyo viwemo kwenye marekebesho ya katiba ya 2013, basi njia sahihi ilikuwa ni kuwasilisha  maombi kwenye mkutano Mkuu wa TFF 13/7/2013 kwa mujibu wa Katiba ya TFF ibara 30 (2006).
 Kwakuwa  TFF haikupeleka  maombi ya mabadiliko haya  na kupitishwa na Mkutano Mkuu wa TFF 2013 hivyo kuyaingiza kwenye katiba ya sasa ya 2013 na kuyaombea usajili kwa msajili  ni kinyume na sheria  na Katiba ya TFF, tafsiri rahisi  ni kuwa  TFF ilitaka  kuonyesha kwa Umma wa Watanzania ya  kuwa serekali kupita msajili wa vyama vya michezo haikuifuta na haikuwa na  mamlaka ya  kuifuta katiba ya Tff  na mabadiliko yake ya Desemba 2012.
4.    UUNDWAJI WA KAMATI KABLA YA MAREKEBISHO YA KATIBA KUSAJILIWA.
TFF iliamua kuunda kamati zake hata kabla katiba haijasajiliwa na Msajili wa vyama vya michezo na vilabu, hii naonyesha jinsi ambavyo mfumo mbovu ulivyozoeleka huko nyuma ambapo msajili alikuwa akisajili  katiba bila kuzingatia mapungufu hivyo kufanya vyama vya michezo kuwa kama mali za watu binafsi  na hata wakati mwingine kumuona msajili kama sehemu ya vyama vyao jambo ambalo Wizara imeamua kulifuta na kuhakikisha taratibu zinafuatwa.
Kwa mujibu wa katiba ya TFF ibara ya37(3)i (2006)  Rais wa TFF anayo mamalaka ya kupendekeza kwa kamati ya Utendaji   majina ya wajumbe wa vyombo vya TFF(TFF Organs) zilizoko kwenye katiba ya TFF ibara ya  44(a,b)(kamati ya nidhamu na Rufaa),ibara 48(mahakama ya usuluhishi,49(Kamati ya Uchaguzi), pamoja na kamati ndogo ndogo (standing Committees) zilizoainishwa kwenye  Ibara ya 39(1)a-i, isipokuwa hana mamlaka ya kuteua wajumbe wa kamati za vyombo ya TFFambavyo havimo kwenye katiba ya TFF (2006) kama   kamati  ya Rufaa ya Uchaguzi, kamati ya Maadili na Kamati ya Rufaa ya Maadili.
 Uteuzi wa Majaji na Wanasheria  waandaamizi kuingia kuongoza kamati ambazo zina utatata wa  kisheria kumeidhalilisha sana idara ya Mahakama na wanasheria kwa Ujumla hali ambayo huenda kwa siku za usoni Majaji / Mahakimu na wanasheria waandamizi  hawataweza kukubali kushirikiana tena  na TFF. Hata hivyo uundwaji wa kamati hizi ni dhahiri ulikuwa ni wa hila kwa kuwateua majaji ili ionekana haki ingetendeka huku TFF ikijua wazi maamuzi yao kwa mujibu wa katiba yanazingatia upigaji wa kura zaidi pale pande mbili zinapopingana kwani ukiachila majaji kwenye kamati hizi wajumbe wanaobaki ni wale wale  ambao kwa mtindo wa Kura wanakuwa wengi(wengi wape)
TFF inaelekeza kuwasilisha malalamiko ya uchaguzi  kwenye vyombo vyake ambavyo ndio  hivyo vilivyo haribu mchakato wa Uchaguzi ambao hadi sas haujafanyika.Katika kuonyesha dhamira isiyo nzuri ya kutaka kuwa na uchaguzi usiokuwa huru na wa haki TFF  imewateua na kuwabadilisha wajumbe ambao kwa sehemu kubwa walishiriki kuharibu mchakato wa uchaguzi uliopita  kwa kuwapa majukumu ambayo kwa njia moja au nyingine bado watashiriki katika mchakato wa uchaguzi unatarajia kufanyika siku za hivi karibuni, mfano ni wajumbe 3 kati ya 5 waliokuwa  kwenye kamati ya Rufaa ya chaguzi ya TFF wamehamishiwa  kwenye Kamati ya Maadili ya TFF(Francis KebweMohamed Mpinga,madundo Mtambo  na mmoja( Murtaza Mangungu  Kamati ya Rufaa ya Maadili,aidha  wajumbe 4 wa kamati ya Uchaguzi Kati ya 5 wamebakishwa kwenye kamati ilie ile na wawili kati yao  wamepandishwa vyeo na kuwa mwenyekiti na Makamu wa Kamati hizo  ambao Hamidu Mbwezeleni (mwenyekiti), Moses Kaluwa (m/mwenyekiti),  Hassan Dyamwale na Kitwana Manara.                           Katika shauri lilifunguliwa mahakama kuu M.A. Ndolanga & others v National Sports Council  and Other [HCT, 1996, TLR 325,Bubeshi,J.]   lililohusu uchaguzi mkuu wa FAT ambalo maamuzi yake hayajawahi kutenguliwa na mahakama nyingine ya juu nchini  mpaka sasa,  matatizo kama haya yalijitokeza na ambapo mahakama pamoja na hoja nyingine ilitaka kujua:)                                                                                                      (i) Kama Kamati ya Usaili ya uchaguzi ya BMT iliundwa kwa kufuata                          misingi ya   sheria?                                                                                            (ii) Kama kamati ya usaili ya Uchaguzi ya  BMT ilifanya kazi kwa                                      kuzingatia  haki asili za kimsingi (Natural Justice and Fair Play)     UAMUZI WA MAHAKAMA ULIMPA USHINDI M.A. NDOLAGA                      Mahakama iliamua kuwa  Vyombo vya maamuzi vya kiutawala wakati wa kutekeleza majukumu yake ambayo yanahitaji kutambuliwa kisheria, vinawajbu wa kutenda kwa kufuata sheria kwa kuzingatia haki za msingi ikwa na maana ya kufuata utaratibu ambao msingi wake utahitaji Uhuru nje ya maslahi na upendeleo kutoka upande wa chombo cha maamuzi kiutawala na haki ya uwazi ya  kusikilizwa kwa wale ambao wataathiriwa moja kwa moja na maamuzi. “it is trite to remark that  an administrative body exercising functions that impinge directly on legal recognized interests, owes it as a duty to act judicially in accordance with the rule of natural justice which  basically means the adoption of  procedure, which fundamentally demand freedom from interest and bias on the part of the administrative body and the right to fair hearing for those who are immediately affected by its decision”(pg 333) 
Kwa kuwa uundwaji na malengo ya  kamati hizi zina walakini kisheria ni wazi uwezekano wa wadau kutafuta msaada wa kisheria mahakamani unaweza kujitokeza kwa kzingatia ukiukwaji mkubwa wa haki za msingi (Natural Justice) na Katiba ya TFF inavyoelekeza            
5.   UKOMO WA MADARAKA WA VIONGOZI WA VYAMA
TFF imehusishwa sana na hila na nia ya kuvuruga uchaguzi ili  waandelee kuliongoza shirikisho kinyume na katibaTFF Ibara ya 33 ya katiba ya tff inazungumzia Ukomo wa madaraka ni miaka 4 na uongozi wao ulikoma Desemba 2012  hivyo uongozi huu kuendelea kuwepo madarakani na kufanya marekebisho ya katiba ni kinyume na katiba ya TFF na sheria ya BMT  ibara 15(1)a. “chama cha mchezo wowote kilichojishirikisha na BMT kitakuwa na wajibu wa kufanya kazi zote za chama kwa msingi wa katiba yake” kwa mujibu wa Katiba ya na kanuni za usajili wa vyama vya michezo kisheria isinge kuwa halali kw a msajili kusajili marekebisho ya Katiba ya TFF kwa kuwa yanapingana na sheria za BMT na Msajili kifungu7(1,2,3,4&5). Vinavyo someka kama ifuatavyo:
·         7(1).Kipindi cha Uongozi wa Chama chochote kitamalizika mara kipindi cha kufanya uchaguzi mwingine kitakapokuwa kimefika kwa mujibu wa katiba ya chama “ ambapo TFFilikuwa Dec 2012
·         7(3) “Viongozi  wanaomaliza muda wao watatakiwa waitisha mkutano mkuu wa Uchaguzi katika Kipindi ha siku 30 kabla ya siku ya ya mwisho ya kipindi cha Uongozi” Jambo ambalo TFF haikulifanya kwa makusudi kwa kingizio cha kupisha mabadiliko ya  katiba kwa njia ya waraka ambayo ni kinuyume cha Katiba Ya TFF.
·         7(4). “Endapo siku 30 zitamalizika baada ya kipindi cha uongozi kumalizika bila ya uchaguzi kufanyika ,na bila ridhaa ya wanachama wa chama husika, viongozi wanaomaliza muda wao watahesabika kuwa wamejivua Uongozi” kwa kuwa Uongozi wa TFF haujapata ridhaa ya kuendelea kuongoza TFF kutoka kwa  wanachama wake. kisheria hawakuwa na mamalaka ya kufanya na kusimamia  mabadiliko ya katiba hivyo msajili kuyakataa ni utekelezaji wa sheria za nchi.
·         7(5). “ Endapo Viongozi wanaomaliza muda wao wamepata ridhaa ya wanachama kuendelea kuongoza baada ya kipindi cha uongozi kumalizika, wanaweza kukiongoza chama husika  kwa kipindi kisicho siku 90 tu baada ya siku ya mwisho ya kipindi cha uongozi. Hata hivyo, ridhaa ya wanachama lazima iwe  imepatikana kabla yatarehe ya mwisho ya kipindi cha Uongozi”.
Kwa mantiki hii Kamati ya Utendaji ilimalizi muda wake 14/12/2012 na haijaahi kupatiwa ridhaa na wanachama wake na hata kama ingepata ridhaa, ridhaa hiyo ilikuwa na ukomo mwezi wa March 2013 , hivyo kamati hii haikuwapo kihalali wakati wa mchakato wa kubadilisha katiba na hivyo kwenda kinyume kanuni za Usajili wa vyama vya michezo  11(1)d “ mabadiliko hayo hayafai kwa kuwa hayakuzingatia Sera ya Michezo ,Sera ya Utamaduni na sheria ya Baraza la Michezo”
6.   HILA ZA  KUVURUGA MCHAKATO WA UCHAGUZI
 TFF imejiongezea muda wa kukaa madarakani zaidi ya Miezi 7 sio kwa sababu yoyote ya msingi zaidi ya mikakati yenye hila ya  kuwaondoa wagombea wasiowahitaji tangu wakati wa kurekebisha katiba kwa njia za hila za waraka ili kuunda kamati zitakazo tekeleza malengo yao  na hadi sasa wanaendelea na mkakati huo ili   kuidhalilisha serekali kwa kuwa ilionyesha msimomo wake wa kutaka wagombea watendewe haki, swali ni vipi watu walioharibu mchakato wa uchaguzi uliolalamikiwa na Wadau na serekeli wapandishwe vyeo tena washiriki katika mchakato huo huo wa uchaguzi na ni vipi watu ambao hawakuwatendea haki wagombea kwa kuwakata na kuwaondoa kwenye mchakato kwa hila  mara ya kwanza watatenda haki tena. Hii ni kinyume na sheria za BMT na  kanuni za msajili Kifugu 11(3)b.kwa kuwa nia ya TFF ni kuwanufaisha wachache
Kwa kuwa Marekebisho ya Katiba ya Tff hayakuzingatia katiba ya TFF na sheria za BMT na Kanuni za Msajili wa Vyama ninaunga mkono uamuzi wa Msajili kukataa kusajili  mabadiliko haya kwa kuzingatia  kanuni za msajili kama ifuatavyo:                                                                                                       
·         11(3)a,  Mabadiliko hayo yanaweza kuhatarisha  usalama na kuvuruga amani  miongoni mwa  wanachama na jamii kwa  ujumla na hivyo kuathiri maeneleo ya chama”.                                                                                                                  
·         11(1)b,  Mabadiliko hayo yanalenga kuwanufaisha wachache”.                              
·         11(1)d,  mabadiliko hayo hayafai kwa kuwa hayakuzingatia Sera ya   Michezo  ,Sera ya Utamaduni na sheria ya Baraza la Michezo.
USHAURI:                                                                                                                1. Kwa Kamati ya Utendaji chini ya L.C Tenga imemaliza muda wake kisheria na  imeshindwa kwa mara nyingine kuandaa katiba ili  kuipeleka TFF katiak Uchaguzi ambao utakuwa wa haki na huri ni vizuri na busara inaelekeza kwa Bwn Tenga na kamati yake   kawajibika kwa kujiuzulu ili kupisha uundwaji wa kamati ya mpito (normalization Committee) kama ilivyofanyika nchi za Sieraleon, Gambia, Cameroon na Tanzania(2001)ili kuandaa  njia huru kuelekea uchaguzi mkuu kupata viongozi wapya.                                                                                                                     2. Kwa kuwa Uongozi uliopa madarakani kwa makusudi umekiuka katiba ya TFF kwa mara ya pili, Msajili atumie kifungu 10(1)a,b (kukiuka katiba ya Chama) za kanuni ya Usajili kuwawajibisha viongozi hawa wa TFF waliomaliza muda  wao.          Kifungu “10(1).b endapo itabainika kuwa kiongozi au viongozi wnaendesha shughuli za chama bila kufuata katiba iliopo au kukiuka kwa makusudi vifungu vya katiba ya chama,msajili anaweza kuchukua hatua ikiwa ni pamoja  kufutwa uongozi kwa kipindi cha uongozi  kilichobaki”.                                                                                               
Michael Richard Wambura.                                                                                                      Nakala:                                                                                                                                            :Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo                                                                                   : Naibu Waziri                                                                                                                     :Msajili wa Vyama vya michezo na Vilabu                                                                          :BMT                                                                



Comments