Na Mwandishi Wetu
MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umempongeza Rais wa
Marekani,Barack Obama na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete kutambua
mchango wa wasanii, wachezaji wa mpira hasa pale walipocheza ngoma na
mpira wa miguu na mpira wa kikapu.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA), Caasim Taalib alisema jana kuwa kitendo cha Rais Obama na mwenyeji wake
Rais Kikwete kucheza ngoma za asili alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (DIA) imeonesha namna ambavyo wanaguswa
na utamaduni wa mtanzania.
Alisema pia kuwa hatua ya Rais Obama kutambua mchango wa
mtanzania,Hasheem Thabit anayecheza mpira wa kikapu ligi ya NBA nchini
Marekanikunaimanish anatambua Tanzania ilivyojaliwa na vipaji
ndiyo maana mchezaji huyo amekuwa nyota kati ya waliosajiliwa kuchezea
timu za
ligi hiyo.
Taalib alisema ni faraja kubwa kuona Rais Obama kuonesha
ufundi wake kumiliki mpira kwa kichwa na kumpasia Rais Kikwete
alipotembelea mitambo ya kufua umeme ya Symbion ambayo ni mshirika wa
Klabu ya Sunderland .
‘SHIWATA baada ya kujua mchango wa Rais Obama iliahirisha
Tamasha la Mastaa Chipukizi lililokuwa lifanyike Jumamosi Juni 29
kijiji cha wasanii Mwanzega Mkuranga ili kutoa nafasi kwa wasanii na viongozi mbalimbali kushiriki kikamilifu katika maandalizi na
mapokezi ya Rais Obama’
ambao wamekamilisha michango ya ujenzi wa nyumba zao katika kijiji chao cha Mwanzega Kimbili, Mkuranga.
Wengine watakaokabidhiwa nyumba zao ni msanii maarufu
nchini, Lumole Matovola ‘Big’ wa Bongo movie ambaye ni mwanachama wa
SHIWATA wangine ni Mwandishi wa Habari, Josephine Moshi, Farida Ndimbo wa
Jeshi la Magereza, Flora Kafwembe wa JKT Mgulani na Nyanza Kisadugwa
wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Comments
Post a Comment