Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi
kutoka Burundi kuchezesha mechi ya kwanza ya mchujo ya Fainali za Afrika kwa
Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Uganda (The
Cranes) itakayofanyika Jumamosi (Julai 13 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Waamuzi hao ni Thierry Nkurunziza atakayepuliza filimbi
wakati wasaidizi wake watakuwa Jean Claude Birumushahu na Pascal Ndimunzigo.
Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni pacifique Ndabihawenimana.
Kamishna wa mechi hiyo Gebreyesus Tesfaye kutoka Eritrea.
Tesfaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Eritrea na mjumbe wa
Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya CHAN.
Comments
Post a Comment