KLABU ya Simba inatarajiwa kuwatambulisha rasmi nyota wake
wapya iliyowasajili kupitia mchezo wake
wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya URA ya Uganda utakaopigwa Julai 20 kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.
Simba kwa sasa ipo
mkoani Katavi ilipokwenda kwenye ziara maalum ya kimichezo baada ya kualikwa na
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ambapo kabla ya kwenda huko ilianzia mkoani Tabora .
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Simba
Evodius Mtawala alisema jana kwamba maandalizi kwa ajili ya mchezo huo
yanakwenda vema ambapo URA inatarajiwa kuwasili nchini Jumatano ijayo.
Alisema pamoja na mchezo huo kutambulisha wachezaji, pia utakuwa
ni sehemu ya kukipima kikosi chake ambacho kipo katika maandalizi ya michezo
yake ya msimu mpya wa Ligi Kuu soka tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Agosti
24 mwaka huu.
“Kama mjuavyo makocha wetu kwa sasa wanaendelea kukinoa
kikosi hivyo kupitia mchezo huo watapata picha halisi ya kuona kasoro zilizopo
katika kikosi na kuzifanya marekebisho,”alisema.
Mpaka sasa Simba imewasajili mshambulijiaji Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ kutoka Mtibwa Sugar
, Kipa Andrew Ntalla kutoka Kagera Sugar,
Beki Adeyum Saleh aliyekuwa anakipiga
Miembeni ya Zanzibar, kiungo Twaha Shekue ‘Messi’ kutoka Coastal union
ya Tanga, Zahoro Pazi kutoka JKT Ruvu
akicheza kwa mkoppo kutoka Azam FC
Aidha, Simba ina
wachezaji wa kimataifa ambao baadhi yao wanawaniwa kusajiliwa wakiwemo James
Kone wa Al Nasri Juba ya Sudan Kusin, beki
Mganda Asuman Buyinza aliyekuwa anacheza
soka la kulipwa nchini Sudan, Tambwe Asuman kutoka Vital’ O ya Burundi, Sammue
Ssenkoon kutoka URA ya Uganda.
Comments
Post a Comment