TIMU ya Ruvu Shooting ya Mlandizi Pwani imejitapa kutwaa
ubingwa wa michuano maalum ya soka ya kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa
Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) inayotarajiwa kuanza Julai 4 hadi 7 katika
viwanja vya Bandari jijini Dar es Salaam.
Tayari kikosi cha wachezaji 18 na viongozi watano wa
maafande hao wameshawasili jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mashindano hayo
yatakayoshirikisha michezo mbalimbali ikiwemo soka itakayoshirikisha timu saba
zikiwemo , Ruvu Shooting, JKT Oljoro, Mgambo Shooting, JKT Ruvu, Kanembwa JKT
na Mlale JKT
“Tupo tayari kwa ajili ya kushiriki michuano hii kikamilifu
ili kushinda na kudhihirisha kwamba sisi ni moja ya timu bora kati ya zile za
majeshi hapa nchini,”alisema
Bwire aliongeza kuwa, kupitia michuano hiyo wanatarajiwa
kushusha jeshi la wachezaji wote wakali ikiwemo wapya ambao wamesajiliwa hivi
karibuni kwa ajili ya kukiimarisha kikosi hicho kwenye ligi kuu bara msimu wa
2013/2014.
Comments
Post a Comment