PINDA AIALIKA SIMBA SC KATAVI, PIA KUWEKA KAMBI NCHINI KENYA

Klabu ya Simba Sports Club imepata mualiko wa Waziri Mkuu kwenda Katavi kucheza mechi ya kirafiki ambapo itaondoka tarehe 13/7/2013 na baada ya hapo itaelekea kucheza mechi za kirafiki Tabora, Mwanza na Musoma kabla ya kuweka kambi fupi Kenya na baadae kushiriki mashindano ya Kilimo yatakayofanyika Kisumu Kenya kuanzia tarehe 31/7/2013 hadi tarehe 4/8/2013. 
Tarehe za mechi husika na timu zitakazocheza dhidi ya Simba SC zitatangazwa hapo baadae. 

Timu ya vijana Simba B inatarajiwa kuondoka tarehe 5/7/2013 kwenda Arusha kwa ajili ya kombe la Rolingstone linalotarajiwa kuanza tarehe 6/7/2013.

Comments