Klabu ya Simba Sports Club imepata mualiko wa
Waziri Mkuu kwenda Katavi kucheza mechi ya kirafiki ambapo itaondoka tarehe
13/7/2013 na baada ya hapo itaelekea kucheza mechi za kirafiki Tabora, Mwanza
na Musoma kabla ya kuweka kambi fupi Kenya
na baadae kushiriki mashindano ya Kilimo yatakayofanyika Kisumu Kenya kuanzia
tarehe 31/7/2013 hadi tarehe 4/8/2013.
Tarehe za mechi husika na timu zitakazocheza
dhidi ya Simba SC zitatangazwa hapo baadae.
Timu ya vijana Simba B inatarajiwa kuondoka
tarehe 5/7/2013 kwenda Arusha kwa ajili ya kombe la Rolingstone linalotarajiwa
kuanza tarehe 6/7/2013.
Comments
Post a Comment