MTIHANI wa kwanza kwa mshambuliaji wa
kimataifa wa Yanga, Mnigeria Ogbu
Brendan utakuwa jumapili ya keshokutwa pale atakapoichezea timu yake dhidi ya
URA.
Yanga na URA zitakwaana siku hiyo
katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki utakaofanyika kwenye uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam.
Brendan aliyetua nchini mapema wiki
hii kwa ajili ya kufanya majaribio na klabu hiyo, hiyo itakuwa mechi yake ya
kwanza na timu hiyo akiwaniwa kusajiliwa.
Kwa sasa Yanga ambao ni mabingwa wa
Ligi Kuu soka Tanzania Bara wapo katika mchakato wa kusaka mshambuliaji ambaye
atashirikiana kwa karibu na Didier Kavumbagu.
Comments
Post a Comment