MIKOA YATAKIWA KUWASILISHA RATIBA COPA COCA-COLA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linavitaka vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kuwasilisha ratiba zao za michuano ya U15 Copa Coca-Cola kabla ya Julai 15 mwaka huu.

Ni vyama vya mpira wa miguu vya mikoa 16 pekee ambavyo ndivyo vimewasilisha TFF ratiba hizo mpaka sasa. Jumla ya mikoa 32 ya Tanzania Bara na Zanzibar inashiriki katika michuano hiyo ya umri chini ya miaka 15 kuanzia ngazi ya wilaya ambapo ngazi ya mikoa inatakiwa kuanza Julai 15 mwaka huu.

Mikoa ambayo tayari imewasilisha ratiba zao ni Arusha, Ilala, Kagera, Kaskazini Pemba, Kaskazini Unguja, Kigoma, Kinondoni, Kusini Pemba, Kusini Unguja, Manyara, Mara, Mjini Magharibi, Morogoro, Singida, Tanga na Temeke.

WASH UNITED YAKABIDHI FULANI 200 KWA KLINIKI YA TFF
Taasisi ya Wash United inayojishughulisha na usaji na utunzaji mazingira imeikabidhi fulana 200 na dola 1,000 za Marekani kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano kati yake na TFF yaliyosainiwa Novemba mwaka jana.

Fulana hizo kwa ajili ya kliniki za kila wikiendi (Jumamosi na Jumapili) zinazoendeshwa na TFF katika vituo 20 nchini kikiwemo cha Karume ikiwa ni sehemu ya mpango wa grassroots unaoshirikisha watoto wa umri kati ya 6 na 17 zimekabidhiwa na Mratibu wa Wash United, Femin Mabachi.

Hafla ya kukabidhi msaada huo imefanyika leo (Julai 9 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF ambapo kwa upande wake ulipokelewa na Ofisa Maendeleo wake Salum Madadi.

Wash United inafadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika lake la maendeleo la GIZ, na hapa nchini moja ya eneo wanalotumia katika kampeni hiyo ili kupambana na magonjwa kama kuhara yanayosababishwa na uchafu ikiwemo kutonawa mikono vizuri, hivyo kusababisha vifo kwa Watanzania ni mpira wa miguu.


Comments