WAKATI mkutano mkuu wa
wanachama wa klabu ya Simba ukitarajiwa kufanyika kesho katika Bwalo la maofisa
wa Polisi Oyesterbay jijini Dar es
Salaam , baadhi ya wanachama wameomba kufanyika kwa
mabadiliko katika baadhi ya vipengele vilivyomo kwenye Katiba ya klabu hiyo ili kuendana na wakati.
Akizungumza kwa niaba ya
wanachama wenzake, Daniel Kamna (100) amesema kwamba, lengo la kutaka
mabadiliko hayo ni kuendana na mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji wa soka hapa
dunaini kwa mujibu wa Mashirikisho ya soka ikiwemo la kimataifa (FIFA), Afrika (CAF) na Tanzania (TFF).
Alivitaja vipengele hivyo ni
pamoja na Ibara ya 26 inayohusu sifa za wagombea ambapo kifungu cha tano
kinasomeka kuwa;mwanachama akitiwa hatiani kwa kosa la jinai asigomnee nafasi
yoyote katika klabu hiyo na wao kuomba mabadiliko hayo yasomeke:asiwe ametiwa
hatiani kwa kosa la jinai lenye adhabu ya kifungo cha zaidi ya miezi sita bila
mbadala wa faini katika miaka mitatu iliyopita.
Kamna aliongeza kuwa, mabadiliko
mengine wanayoomba ni baadhi ya majina ya vyeo ya viongozi ambapo badala ya
Mwenyekiti aitwe Rais, Makamu Mwenyekiti aitwe Makamu wa Rais.
“Pia mkutano mkuu wa uchaguzi
uwe na mabadiliko yafuatayo kwa viongozi wa kuchaguliwa wawe ni Rais na Makamu wa Rais”, alisema
Aliongeza kuwa katika
kipengele cha kamati ya utendaji;Ibara ya 28 inayozungumzia muundo, wameomba
isomeke kwamba:Kamati ya utendaji ya Simba Sports Club itaundwa na Rais, Makamu
wa Rais, Wajumbe saba ikiwemo mwanamke mmoja wa kuteuliwa na Rais na mjumbe
mmoja wa kuteuliwa akitokea Baraza la Wazee.
Comments
Post a Comment