JUHUDI za Klabu za Yanga na
Simba katika kumfukuzia mshambuliaji mahiri
Hassan Dilunga wa timu ya Ruvu Shooting
ya Pwani, zimeingia dosari baada ya nyota huyo kuongezewa mkataba.
Mbali ya kufanikiwa
kumbakisha Dilunga, Shooting pia imemsajili kiungo Juma Seif ‘Kijiko’ aliyewahi
kuichezea Yanga kabla ya kuhamia kwa mkopo African Lyon ambayo imeshuka daraja.
Kijiko anaungana na nyota
mwingine kinda, Cosmas Ader, aliyekuwa akiwaniwa na timu kadhaa zikiwemo kongwe
za
Simba na Yanga.
Kabla ya kutua Shooting, Ader
alikuwa kicheza kwa mkopo Lyon akitokea klabu ya Azam FC.
Ofisa habari wa Shooting, Masau
Bwire ameiambia Sports Lady kwamba kuwa, wamekamilisha usajili wa nyota wa msimu ujao wa 2013/14.
Alisema usajili limefanyika
kwa umakini ili kuwa na kikosi bora kitakacholeta ushindani mkubwa kwenye ligi hiyo inayotazamiwa kuanza Agosti 24.
“Tunashukuru kwa kiasi
kikubwa, tumefanikisha usajili wa kikosi chetu kulingana na mahitaji ya timu,
naamini tutatoa ushindani mkubwa kwenye msimu ujao,” alisema.
Nyota wengine waliosajiliwa
Shooting na timu zao kwenye mabano, ni Jerome Lambele (Azam) aliyekuwa akicheza
kwa mkopo Ashanti United na Juma Nade (Kagera
Sugar).
Comments
Post a Comment