Simba
Sports Club inatarajia kuwa na wiki ya kijamii kuanzia tarehe 5/8/2013 hadi
tarehe 11/8/2013 na programu itakuwa kama
ifuatavyo:-
5/8-KUTEMBELEA
KITUO CHA WATOTO YATIMA NA KUTOA MSAADA
6/8-KUTEMBELEA
WAGONJWA WASIOJIWEZA HOSPITALI NA KUTOA MSAADA
7/8-KUHUDHURIA
KOZI/SEMINA ILIYOANDALIWA NA WADHAMINI TBL PAMOJA NA KUTEMBELEA KIWANDA CHA TBL
8/8-SIMBA
DAY
9/8-KUTEMBELEA
SHULE YA MSINGI NA KUHAMASISHA MICHEZO MASHULENI
10/8-KUTEMBELEA
MEDIA HOUSE ILI KUENDELEZA MAHUSIANO MEMA NA
VYOMBO VYA HABARI
11/8-KUFANYA
DUA NA IBADA KLABU KATIKA IMANI ZOTE (KUWAOMBEA REHEMA WALIOTANGULIA, KUOMBA
MEMA KATIKA MSIMU UJAO).
MAENDELEO
YA MPANGO MKAKATI WA KLABU (STRATEGIC PLAN)
Open university wameishatuma draft ya kwanza ya
Strategic Plan ambapo Kamati ya Utendaji mnamo tarehe 13/7/2013 itakutana na
kamati ya marejeo kuipitia strategic plan hiyo ili kuijadili kwa mapana kurudisha
mrejesho kwa ajili ya kuandaa draft ya mwisho tayari kuingizwa Mkutano Mkuu wa
wanachama.
SUALA LA MATIBABU YA
KIGI MAKASI
Timu ya kitabibu ya Simba Sports Club ipo katika
mchakato wa kupata “appointment” nchini India kwa ajili ya kumsafirisha KIGI
MAKASI kupata matibabu zaidi nchini humo baada ya kupata rejesho la daktari wa
timu. Mchezaji husika anatarajiwa kuwa nchini India mwanzoni mwa mwezi ujao.
IMETOLEWA NA
EZEKIEL KAMWAGA
AFISA HABARI
SIMBA SPORTS CLUB
4/7/2013
Comments
Post a Comment