- Mechi za fainali ambazo mgeni rasmi atakuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makala zitachezwa kuanzia saa 7.30 mchana kwa wasichana wakati ile ya wavulana itaanza saa 9.30 alasiri.
Nusu fainali za mashindano hayo ambazo pia zinaonekana moja
kwa moja SuperSport zinachezwa leo (Julai 5 mwaka huu). Kwa upande wa wasichana
ni kati ya timu za Kinondoni na Kigoma wakati Ilala inaumana na Temeke.
Kwa upande wa wavulana nusu fainali ya kwanza ni kati ya
Mwanza na Ilala ambapo baadaye itafuatiwa na nyingine kati ya Morogoro na
Kinondoni. Mechi za kutafuta mshindi wa tatu zitachezwa kesho asubuhi (Julai 6
mwaka huu).
Comments
Post a Comment