KLABU ya soka Coastal Union ya Tanga ‘Wagosi wa Kaya’
imevunja ukimya na kukana kumsajili ama kuwa na mpango wa kumsajili aliyekuwa
kipa wa Simba, Juma Kaseja.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union, Nassor Bin Slum amesema kwamba Kaseja hana nafasi ndani ya klabu hiyo
kutokana na ukweli kwamba tayari wana makipa watatu wanaoweza kukidhi mahitaji
ya klabu hiyo.
“sisi tunasajili kwa mipango na hatuangalii majina kwani
katika safu ya makipa tuna Said Lubawa tuliyemsajili
toka JKT Oljoro,yupo Shaban Kado, pia tunaye Mansoor Mansoor ambaye
tumempandisha kutoka timu B,”alisema
Bin Slum aliongeza kwamba watu walijenga imani kuwa timu yao itakuwa sebule ya wachezaji
waliotemwa Simba baada ya kusajali Haruna Moshi ‘Boban’ na Juma Nyoso, lakini
ukweli ni kwamba nyota hao walisajiliwa kutokana nas ytimu yao kuhitasji
wachezasji wa nafasi hizo.
“Baada ya kuwanyakua Bonas nas Nyoso mengine yakazushwa mara
tunamsajili redondo (Ramadhan Chombo), mara Amir Maftah yote sijui yalitoka
wapi, sisi tunasajili kwa malewngo maalum,”aliongeza.
Comments
Post a Comment