MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara timu ya Yanga kesho inatarajiwa kuanza mazoezi rasmi kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi
hiyo pamoja na michuano ya kimataifa.
Kizuguto alisema timu hiyo itafanya mazoezi yake jijini kwa
siku tatu mfululzio kabla ya siku ya ijumaa kusafiri kuelekea jijini Mwanza kwa
ajili ya ziara maalum ya kimichezo itakayoambatana na shamrashamra za kupeleka
ubingwa wa ligi hiyo kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa.
Alisema siku ya Jumamosi timu hiyo itashuka katika dimba la
CCM Kirumba kukwaanma na mabingwa wenzao wa Uganda , Kampala City Council (KCC),
kabla ya kurudiana Jumapili mjini Shinyanga, mchezo utakaopigwa dimba la
Kambarage.
“Baada ya michezo hiyo, jumatatu timu itaelekea mjini
Tabora kwa ajili ya mchezo mmoja wa kirafiki ambao utapangwa na waandaaji na
kisha kikosi kitarejea jijini Dar es salaam kuendelea na maandalizi ya msimu
mpya wa ligi,”alisema.
Comments
Post a Comment