KLABU za APR ya Rwanda na Gor Mahia ya
Kenya zipo katika harakarti za kumwania aliyekuwa kipa namba moja wa timu ya
Simba, Juma Kaseja, imefahamika.
Habari za uhakika ambazo Sports Lady Blog imezinyaka zinasema viongozi wa
timu hizo wameshaanza mazungumzo na Kaseja ili kumsajili kwa msimu ujao katika
nchi hizo.
Mdau mmoja wa soka ambaye yupo karibu
na uongozi wa timu hizo, alidokeza jana kwamba, kwa nyakati viongozi wa timu
hizo mbili, wamekuwa kwenye harakati za kumsaka Kaseja, wakiamini bado ni kipa
mwenye uwezo mkubwa langoni.
Licha ya kutemwa kwenye kikosi cha
Simba kwa msimu ujao, Kaseja bado kipa namba moja wa timu ya soka ya Tanzania,
Taifa Stars chini ya kocha wake Kim Poulsen, raia wa Denmark.
Habari zaidi zinasema, klabu ya APR iliyofika
fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashabiki na Kati-Kagame Cup na kufungwa na
Vital’o wiki moja iliyopira nchini Sudan, inapewa nafasi kubwa ya kumpata kipa
huyo.
Hayo yanatokea huku Kaseja akiwa kwenye
kambi ya timu ya Stars inayojiandaa na mechi ya kuwania tiketi ya Fainali za
Afrika kwa Nyota wa Ndani –CHAN dhidi ya Uganda itakayopigwa Julai 13, Uwanja
wa Taifa Dar es Salaam.
“Ujue baada ya Simba kutangaza kuachana
na Kaseja, kuna timu nyingi hasa za nje zimeonesha nia ya kutaka kumsajili
lakini mpaka sasa ni APR na Gor Mahia ndio wako makini zaidi na mchakato huo,”
kilisema chanzo hicho.
Hivi karibuni uongozi wa Simba
ulitangaza kuachana na Kaseja aliyekuwa kipa wake namba moja na nahodha wa timu
hiyo bila ya kuweka rasmi sababu za kuachana naye baada ya kumaliza mkataba
wake, Meii.
Aidha, baadhi ya klabu za Ligi kuu
ambazo zilikuwa zikitajwa kumuania nyota huyo aliyeitumikia Simba nazo zilidai
hazina mpango wa kumsajili kwani zinamakipa wa kutosha.
Comments
Post a Comment