SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema
linasubiri tamko rasmi la Serikali juu ya ushiriki wa timu za Simba na Yanga
katika michuano ya klabu bingwa Afrka Mashariki na Kati ‘Kombe la Kagame’
iliyopangwa kufanyika Juni 18 hadi Julai 2 nchini Sudan.
Hatua hiyo inafuatia kuwepo kwa machafuko
katika jimbo la Darfur nchini humo ambako tayari baadhi ya timu zimetangaza
kutoshiri mashindano hayo kwa hofu ya hali ya kiusalama.
Kutokana na hali hiyo, Serikali kupitia
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe alisema hivi karibuni kwamba
haoni kama kuna umuhimu wa Tanzania kushiriki katika michuano hiyo.
Rais
wa TFFLeodger Tenga amesema leo kwamba tayari wameshakutana na viongozi wa
serikali yaani Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo pamoja na Wizara ya
Mambo Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa ajili ya kuzungumzia suala hivyo.
Alisema katika kikao baina ya Tff na Serikali
waliwasilisha taarifa za hali halisi ya usalama ulivyo nchini Sudan pamoja na
uhakika wa timu kushiriki mashindano hayo hivyo kilichobaki ni serikali
kujiridhisha kwa kuhakikisha kama hali ni shwari ama la na kutoa tamko lake.
“Serikali ndiyo yenye mamlaka ya mwisho juu ya
ushiriki wetu kwenye Kombe la Kagame na tunachukulia uzito kauli ya Waziri
ndiyo maana tumekuwa katika majadiliano,tunasubiri maamuzi ya serikali kwani
hili sio suala la TFF na hakuna mvutano katika hili na tunatumaini serikali
itatoa ruhusa,”alisema Tenga.
Tenga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la
Vyama vya Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) aliongeza kwamba awali mashindano
hayo yalikuwa yafanyike nchini Ethiopia kabla ya kusema hawako tayari kuyaandaa
na ndipo Sudan ikaamua kubeba jukumu hilo.
“Kabla ya kuwakubalia suala la machafuko
lilikuja mezani lakini walituhakikishia hali ni shwari na pia masuala ya
malazi, usafiri n.k yapo sawa, hivyo Cecafa tukamtuma katibu wetu huko na
alipokwenda kufanya ukaguzi aliliridhika na yale tuliyoambiwa hivyo
tukapisha,”alisema
Aidha, Tenga aliishukuru Sudan kukubali na
kujitolea kuwa wenyeji wa michuano hiyo kutokana na ukweli kwamba ni vigumu
kuyaendesha masahindano haya, pia maendeleo ya soka hayaji hivihivi.
Hata hivyo, Tenga alisema hana taarifa ya
kujitoa kwenye michuano hiyo zikiwemo timu mwenyeji El Merreikh na Al Hillal na
kusema kuwa atalifanyia kazi,huku kuhusiana na Tusker ya Kenya kujitoa kwenye
michuano hiyo akisema huwezi kumlazimisha mtu kucheza.
Comments
Post a Comment