WAKATI Serikali ikibariki rasmi kuwa timu za Simba, Yanga na
Falcon ya Zanzibar ,
hazitashiriki michuano inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika
Mashariki na Kati (Cecafa), Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema
haliwezi kupingana uamuzi huo.
Jana bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Amos Makalla (pichani), alitoa kauli rasmi ya serikali, wakati
akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Sumve, Richard Ndassa.
Ndassa katika swali lake, alitaka kujua msimamo wa serikali
kama timu za Tanzania
zitashiriki michuano hiyo ambayo iko shakani, kutokana na baadhi ya mataifa
kuanza kujitoa kutokana na hali duni ya usalama nchini Sudan .
Akijibu swali hilo , Makalla
alisema, ni kweli kumekuwa na taarifa za kutokuwa na usalama nchini Sudan
na kwamba, Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe alishalitolea ufafanuzi.
“Sisi ndani ya serikali tuna taarifa za kutosha kuwa Sudan
Kusini hakuna usalama na nchi nyingine zimeendelea kujitoa, hivyo msimamo wetu kama serikali, hatuwezi kupeleka timu sehemu isiyo na
usalama,” alisema Makalla.
Juni mosi mwaka huu, Waziri Membe wakati akihitimisha hotuba
ya bajeti ya wizara yake, alisema kwamba, anashangaa kuona Sudan ikipewa uenyeji wa michuano
hiyo licha ya kuwa na usalama mdogo.
Alisema kwa mujibu wa sheria za kimataifa, kwenye nchi zenye
machafuko ili michuano kama hiyo iweze kufanyika ni lazima sehemu husika
wanakofikia wachezaji na maofisa wengine kuwe na magari maalumu ya kuzuia
risasi (bullet proof) ya kuwabeba kutoka uwanja wa ndege hadi sehemu
wanakokwenda.
Waziri Membe, alihoji busara iliyotumiwa na Cecafa kuteua
nchi hiyo kuwa mwenyeji wa michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Juni 18.
Akizungumzia
hali hiyo jana, Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah, alisema, Serikali ndiyo
yenye mamlaka ya mwisho juu ya suala hilo na kama imeona hali hairuhusu kwa Simba na Yanga kwenda
huko, hawana budi kuheshimu uamuzi hao.
“Haya
mashindano yapo chini ya Cecafa, hivyo hatuwezi kuyazungumzia zaidi, lakini kama wasimamizi wa soka nchini hatuna budi kufuata
maelekezo ya Serikali, kwani ndiyo ina uamuzi wa mwisho,” alisema
Mwalusako
aliongeza kwamba, timu yake imekuwa katika maandalizi si kwa ajili tu ya ushiriki
wa michuano hiyo, kwani kuna ligi kuu, klabu bingwa ya Afrika na hata mechi
kadhaa za kirafiki.
Naye
Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ alisema, wakipata
rasmi taarifa ya Serikali, uongozi utakutana na kuamua nini cha kufanya.
Comments
Post a Comment