Klabu ya Everton, imekata ombi lililowasilishwa na
Manchester United la kutaka kumsajili mlinda lango wake Leighton Baines kwa
kitita cha pauni milioni kumi na mbili.
Kocha mpya wa Manchester David Moyes ambaye alisajiliwa hivi
majuzi kutoka kwa klabu hiyo ya Everton alitaka kumasjili mchezaji huyo ili
kuimarisha safu yake ya ulinzi.
Siku chache tu baada ya kusajiliwa kama kocha wa Manchester
United Moyes, alitangaza wazi wazi kuwa nia yake kuu ni kumsajili mechaji huyo
mwenye umri wa miaka ishirini na minane.
Ripoti zinasema Manchester United inajianda kuwasilisha ombi
lingine baada ya kuongeza fedha za kumsajili.
Hata hivyo, wasimamizi wa Everton, wamesema kuwa hawana nia
yoyote ya kumuuza mchezaji huyo.
Kocha mpya wa Everton, Roberto Martinez kwa upande wake
amesema anataka mchezaji huyo ambaye aliteuliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka
msimu uliopita kusaini mkataba mpya.
Uamuzi huo wa Moyes wa kutaka kumsajili, Baines, huenda
ukahujumu nafasi ya mcheza kiungo wa Manchester United Patrice Evra mwenye umri
wa miaka thelathini na miwili.
CHANZO:BBC SWAHILI
CHANZO:BBC SWAHILI
Comments
Post a Comment