MISS TEMEKE WAANZA KUJINOA LEO TCC CLUB CHANG'OMBE

VIMWANA 16 wa kanda ya Temeke, wameanza kujinoa leo(Juni 17) kwenye klabu ya TCC Chang'ombe, tayari kwa kinyanga'nyiro kitakochafanyika Julai 5, mwaka huu katika ukumbi huo.
Idadi hiyo ya warembo ni kutoka Kigamboni, Kurasini na Chang'ombe ambao wanawania taji linaloshikiliwa na Miss Tanzania namba tatu, Edda Sylvester ambaye atakuwa mmoja wa wakufunzi katika kambi hiyo, ambayo pia inasimamiwa na Suzy Mwenda na Shadya Mohamed.
Mbali ya hao, pia kutakuwa na jopo na wakufunzi wa dansi, litakaloongozwa na Bokilo na Charles yote katika kuhakikisha shoo ya mwaka huu, itaendana na ubora wa warembo wanaoshiriki shindano hilo, ambapo kwa hakika Redds Miss Tanzania mwaka huu, bila shaka atatokea katika kanda hiyo, yenye historia ya mafanikio.
Temeke, imewahi kutoa warembo kadhaa miaka ya nyuma waliopata mafanikio katika mashindano hayo, mitindo na kazi nyingine hasa kupata uzoefu wa kujiamini katika njanja mbalimbali.
Miongoni mwao ni Miriam Odemba(1997) aliyepata kuiwakilisha Tanzani katika fainali za mitindo zilizofanyika Nice Ufaransa na kupata mkataba wa Elite Model Look, baadaye kufakinikiwa kutwaa nafasi ya pili ya Miss Earth World, zilizofanyika China.
Pia, Temeke ilimtoa Happines Millen Magesse(2001), na kutwaa taji la Miss Tanzania na kwa sasa anang'ara sana katika tasnia ya mitindo katika nchi za Marekani, Afrika Kusini na barani Afrika kwa ujumla. 2003 Temeke ilimtoa Miss Tanzania, Sylvia Bahame na 2006 kuwatoa Jokate Mwegelo na Irene Uwoya.
Jokate alitwaa taji la Miss Temeke mwaka huu na pia kushika nafasi ya pili Miss Tanzania na pia kushinda taji la ubalozi wa Redd's na gazeti la Citizen. Uwoya ambaye alikuwa mshindi wa pili Temeke alishika nafasi ya nne kwenye Miss Tanzania mwaka huo. Genevieve Mpangala mwaka 2010 alitwaa taji la Miss Temeke baadaye kushinda taji la Miss Tanzania.
Nafasi nyingine za juu zilizowahi kutwaliwa na warembo kutoka Temeke ni pamoja na Irene Kiwia, mshindi wa nne Miss Tanzania mwaka 2000, Regina Mosha mshindi wa nne Miss Tanzania mwaka 2002, Cecylia Assey mshindi wa pili Miss Tanzania 2004, Queen David mshindi wa tatu mwaka 2007 na Edda Sylvester mshindi wa tatu Miss Tanzania akiwa anashikilia taji la Redds Miss Temeke.
Shindano hilo, linalotarajiwa kuwa na burudani ya kipekee limedhaminiwa na kinywaji cha Redd's, Dodoma Wine, Jambo Leo, Blogu ya Wananchi (Le Mutuz), Fredito Entertainment, Kitwe General Traders na CXC Africa tours & Safaris.
Warembo wa Redds Miss Temeke 2013
1-Axsaritha Vedastus,2-Belinda Paul,3-Darling Mmary,  4Esther Muswa, 5-Hyness Oscar, 6-Irene Rajab, 7-Jamila Thomas, 8-Latifa Mohamed,9-Margreth Gerald, 19-Margreth Olotu,11-Mey Karume ,12-Mutesi George, 13-Naima Ramadhan, 14-Narietha Boniface, 15-Stella Mngazija               
16-Svtlona Nyameyo                                       

Comments